Searching...
Monday, October 13, 2014

OZIL KUONDOKA ARESNAL MWEZI JANUARY, BAYERN MUNICH WAONYESHA DALILI ZA KUMTAKA

Mesut Ozil's last game for Arsenal may have been against Chelsea at Stamford Bridge last Sunday
Ozil amekuwa hana namba ya kudumu kunako Emirates; Wenger amekuwa akimchezesha katika nafasi anayo jiskia yeye kumchezesha. Hicho kitendo haikimfurahishi Ozil na ndiyo maana anaona ni vyema kuhama na kwenda katika klabu itakayomtumia kulingana na nafasi anayo mudu kucheza
Tetesi zinasema kwamba mshambuliaji wa Arsenal, Mesut Ozil ataondoka katika klabu ya Arsenal mwezi January, hii ni kutokana na meneja wa klabu hiyo, Arsenal Wenger  kuendelea kumchezesha katika nafasi asiyoipenda uwanjani (kiungo).

Kwa sasa, Ozil yuko nje ya dimba kwa takribani miezi mitatu kwa sababu ya jeraha la goti lililompata wakati akiwa katika kambi ya timu yake ya taifa iliyokuwa ikijianda kwa mechi ya kusaka tiketi za kushiriki ligi ya mabingwa wa bara la Ulaya dhidi ya Poland ambayo ilichezwa jana na Poland kuibuka na ushindi wa magoli 2-0.
Ingawaje Arsene Wenger hana tabia ya kuuza wachezaji katika kipindi cha dirisha dogo la usajili, wachambuzi wa mambo wanaamini suala la masilahi ndilo litaamua zaidi kama Wennger atakubali kufanya biashara hiyo au la mwezi Januari, 2014.
Klabu ya Bayern Munich inatajwa kuwa mstari wa mbele kutaka kumchukua Ozil kwa dau la pauni milioni 30 endapo wabeba mitutu watakubali kumuachia.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!