Searching...
Monday, October 13, 2014

MSHAMBULIAJI WA CHILE APOTEZA MENO MAWILI UWANJANI TIMU YAKE IKISHINDA 3-0 DHIDI YA PERU.

Former Cardiff City midfielder scored during Chile's 3-0 victory over Peru in an international friendly
Rafu za aina hii zinapingwa sana na sheria za mpira wa miguu na ndiyo maana mwamuzi wa mchezo wa jana kati ya Chile dhidi ya Peru, J.Quintana alimtoa nje Ricardo Cruzado (jezi nyeupe) kwa kadi nyekundu. Hiyo ndiyo rafu iliyomvunja Gary medel meno mawili.
Ulikuwa ni mpepetano wa kutumia nguvu nyingi sana kati ya timu ya taifa ya Chile dhidi ya timu ya taifa ya Peru ambapo, mshambuliaji wa Chile na klabu ya Ineter Milan kwa sasa, Gary Medel amejikuta akipoteza meno yake mawili baada ya kupigwa kiwiko "kipepsi" na mchezaji wa Peru, Ricardo Cruzado wakati wakigombania mpira wa juu.

Magoli mawili ya Chile yalifungwa na mshambuliaji Eduado Vagas kwenye dakika ya 28 na 53, wakati goli la tatu lilifungwa na  Medel dakika ya 34, magoli ambayo yalifanya Chile kutoka kifua mbele uwanjani baada ya ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Peru. 
Gary Medel was left spitting blood after having two teeth broken by Ricardo Cruzado's elbow
Kwa mujibu  wa taarifa kutoka kwa dakitari wa timu ya taifa ya Chile, Giovanni Carcuro, zinasema kwamba, mara baada ya tukio hilo, Medel alionana na mtaalam wa meno kwa ajili ya kushughulikia jeraha lake, na muda mfupi atakuwa sawa.
Timu ya taifa ya Peru itabidi ijilaumu yenyewe kwa uzembe mkubwa waliokuwa nao uwanjani, ambao uliwafanya pia wakosea penati dakika ya 20 ya mchezo huo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!