marquee

WELCOME URARY95 BLOG ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE FOR MORE INFORMATION CONTACT US TELEPHONE: +255714457899 E-mail:moemyad@yahoo.com YOU ARE WELCOME | KARIBU URARY95 BLOG TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI SIMU: +255714457899 E-mail: moemyad@yahoo.com | NYOTE MNAKARIBISHWA. | DO YOU NEED TO CREATE BLOG CONTACT US CLICK HERE | UNAHITAJI KUFUNGUA BLOG WASILIANA NASI BOFYA HAPA

TAFUTA CHOCHOTE BLOGUNI HAPA

Loading...

Friday, June 1, 2012

FAO yataka njaa na utapia mlo zitokomezwe Maendeleo endelevu hayapatikani kukiwa na njaa

kilimo cha mboga
Picha AFP
Kilimo cha mboga
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa- FAO, linasema maendeleo endelevu hayawezi kufikiwa  hadi pale njaa na utapia mlo zitakapotokomezwa. Katika ripoti iliyotolewa Jumatano  mkuu wa shirika hilo la FAO Jose Graziano da Silva, alisema lengo la maendeleo  endelevu kamwe haliwezi kufikiwa ikiwa takriban mmoja kati ya watu saba duniani anakabiliwa na njaa au utapia mlo . Alitoa mwito wa kuongeza  uzalishaji wa chakula na wakati huo huo kulinda mazingira ili dunia iweze kukidhi mahitaji ya chakula kwa watu wanaokisiwa kufikia bilioni tisa  ifikapo mwaka wa 2050. FAO linasema kufanikisha lengo hilo lazima uwezekazji katika kilimo uongezwe kwa asili mia 60 katika miongo ijayo. Shirika hilo linaongeza kuwa robo tatu ya watu maskini duniani huishi vijijini ambapo wengi wanategemea kilimo kwa maisha yao. Ripoti  ya shirika  hilo la FAO imetolewa kabla ya mkutano ujao wa Umoja wa Mataifa  unaotazamiwa kufanyika mjini Rio De Janeiro kuanzia Juni 20 hadi 22. Mchumi wa ngazi ya juu wa shirika  hilo la chakula na kilimo duniani aliiambia sauti ya Amerika kuwa ajenda kuu ya  mkutano huo itakuwa kutokomeza njaa duniani.

Callixte Nzabonimana ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Fuvu za vichwa vya Wanyarwanda waliouawa mwaka wa 1994
Mahakama ya uhalifu wa kivita kwa ajili ya Rwanda imemhukumu kifungo cha maisha jela afisa wa zamani wa Rwanda Callixte Nzabonimana kwa mauaji  ya halaiki. Mahakama hiyo ya kimataifa  kwa ajli ya Rwanda ilisema waziri huyo wa zamani alichochea mauaji ya watu  kati ya 15 hadi 60 wa  kabila la Tutsi mwezi  Aprili mwaka wa 1994 katika eneo la Nyabikenke. Ilisema pia kuwa alichochea watu mara tatu hadharani mwezi huo kuwauwa Watutsi na akaingia kwenye makubaliano ya kuwauawa watu wa kabila hilo na serikali ya muda ya Rwanda wakati huo. Nzabonimana alikuwa waziri wa maswala ya vijana wa Rwanda  katika serikali ya muda iliyoundwa mwaka wa 1994. Alikamatwa mwezi Februari nchini Tanzania na kukabidhiwa mahakama ya kimataifa ya uhalifu kwa ajili ya Rwanda yenye makao yake mjini Arusha, Tanzania. Wanamgambo wa Kihutu inakisiwa waliuawa watu laki 8 wa kabila la Tutsi na Wahutu wenye msimamo wa kadri wakati wa mauaji ya halaiki  mwaka  huo wa  1994. Mahakama hiyo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ilibuniwa kwa ajili ya kusikiliza kesi dhidi ya wahusika wakuu wa mauaji ya halaiki ya Rwanda.

Terry aadhibiwa na UEFA

Mlinzi wa klabu ya Chelsea, John Terry, atazikosa mechi mbili msimu ujao utakapoanza wa mechi za Ulaya, kufuatia adhabu ya UEFA kumzuia asicheze katika mechi tatu.
John Terry
Aongezewa adhabu kwa kumpiga kwa goti mchezaji wa Barcelona
Tayari aliikosa fainali dhidi ya Bayern Munich, baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo wa nusu fainali, wakati Chelsea ilipopambana na Barcelona.
Lakini UEFA sasa imeamua kumuongezea adhabu, kwa kumkataza kucheza katika mechi mbili zaidi.
Terry pia hatakuwepo katika mechi ya Kombe la Super dhidi ya washindi wa ligi ya Europa, Atletico Madrid ya Uhispania, itakayochezwa mwezi Agosti, na vile vile mechi ya kwanza ya Chelsea katika hatua ya makundi ya kufuzu kwa ligi ya klabu bingwa Ulaya.
Terry na Chelsea wana muda wa siku tatu kuamua ikiwa watakata rufaa au la kufuatia uamuzi huo.
Terry, mwenye umri wa miaka 31, alitolewa kadi nyekundu na mwamuzi, kufuatia kushindilia goti lake dhidi ya mchezaji wa Barca, Alexis Sanchez, pasipo hata mpira kuwa karibu, wakati Chelsea ilikuwa tayari imefungwa bao 1-0 usiku huo.
Aliwaomba msamaha wenzake kwa kuwaletea fedheha.
Hata hivyo licha ya kuondolewa Terry katika mechi hiyo, hatua hiyo haikuinyima Chelsea ushindi, kwani hatimaye iliondoka kwa sare ya 2-2, na katika uwanja wa Nou Camp, waliibuka washindi kwa jumla ya magoli 3-2.
Kisha baada ya hapo walipata ubingwa wao wa kwanza katika fainali ya klabu bingwa, licha ya kuwakosa wachezaji mahiri Terry, Ramires, Branislav Ivanovic na Raul Meireles.

Mauwaji Syria- Uhalifu dhidi ya Binadamu

Syria moto
Syria moto
Mauwaji ya zaidi ya raia 100 katika mji wa Houla nchini Syria wiki iliyopita huenda ukaelezewa kama uhalifu dhidi ya binadamu, kwa mujibu wa Kamishna wa Haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa.
Navi Pillay ameisihi jumuia ya kimataifa itumie kila njia na juhudi kuhakikisha wahusika wa vitendo hivyo wanawajibika.
Bw.Pillay aliyasema haya wakati akihutubia Kikao cha dharura cha Baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa.
Hapo awali, wanaharakati wa upinzani walisema kua kuna mauwaji mengine ya raia yaliyofanywa na wana mgambo wanaoungwa mkono na serikali.
Mauwaji Syria
Mauwaji Syria
Wafanyakazi 13 wa kiwanda kimoja waliamrishwa kutoka ndani ya basi walilokua wakisafiria na kuuawa na ''Shabiha'' Jina la wanamgambo hao wanaoiunga mkono serikali siku ya alhamisi huko al Buwaida al Sharkiya, karibu na mji ulio magharibi mwa nchi wa Qusair.
Video kadhaa zilizotumwa kupitia mtandao zilionyesha maiti zenye majeraha ya risasi zilizopigwa kichwani na kwenye tumbo, ikiashiria walipigwa risasi na mtu aliye karibu nao.
Madai hayo ya wanaharakati hayana uthibitisho huru, lakini wasimamizi wa Umoja wa Mataifa walioko huko Syria waliweza kuthibitisha madai kama haya mara mbili katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.
Baraza la Haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, likiwa ndilo shirika la kiwango cha juu duniani, lilianza mkutano wa dharura kujadili ghasia za nchini Syria. Hii ni mara ya nne kwa Baraza hili kujadili Syria tangu vuguvugu la kumpinga Rais Bashar Al Assad lianze mnamo mwezi Machi mwaka 2011.

Thursday, May 17, 2012

WANAMICHEZO,WANAMUZIKI WAMLILIA MAFISANGO


Wachezaji Haruna Niyonzima wa Yanga kushoto na Uhuru Selemani wa Simba wakisikitika wasijue la kufanya baada ya kushuhudia mwili wa mchezaji mwenzao marehemu Patrick Mafisango katika chumba cha kuhifadhia maiti muhimbili leo.
Mbunge wa jimbo la Korogwe CCM Steven Ngonyani Prof Maji Marefu akizungumza na wanahabari hospitalini hapo kuelezea masikitiko yake juu ya kifo cha mchezaji huyo.
Haruna Moshi akitoka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti huku akilia kwa uchungu baada ya kuhakikisha kweli mwenzao Patrick Mafisango amefariki.
Hapa Haruna Moshi akihojiwa alijaribu kuongea lakini akashindwa.
Mchezaji Uhuru Selemani akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na mmoja wa waombolezaji.
Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na Mchezaji haruna Niyonzima wa Yanga, Pawasa amesema jana walikuwa naye kwenye muziki katika klabu ya Maisha Oysterbay wakati bendi ya Akudo Impact ikifanya onyesho klabuni hapo na marehemu alimuaga kwamba anaenda nyumbani baadae akapigiwa simu kwa simu ya marehemu akiambiwa mwenye simu hii amefariki dunia kwa ajali.
Boniface Pawasa kushoto, Uhuru Selemani wakilia.
Uhuru Selemani akisalimiana na wanamuziki wa bendi ya Akudo Impact ambao pia wameelezaea masikitiko yao kwani wamesema marehemu walikuwa naye usiku wa kuamkia leo katika klabu ya Maisha ambako walikuwa wakifanya onyesho lao.
Aliyewahi kuwa mchezaji wa timu ya Simba Mrundi Ramadhana Wasso akihojiwa na waandishi wa habari kuelezea masikitiko yake kutokana na msiba huo.
Mashabiki wa Simba wakiwa katika hospitali ya Muhimbili kwa masikitiko makubwa kwa kuondokewa na mchezaji wao kipenzi.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili leo asubuhi.

PATRICK MAFISANGO WA SIMBA AFARIKI DUNIA


HABARI TULIZO ZIPOKEA ASUBUHI HII ZINAPASHA KUWA MSHAMBULIAJI WA KIMATAIFA WAMABINGWA WA SOKA TANZANIA BARA SIMBA SC, PATRICK MUTESA MAFISANGO, NA MCHEZAJI WA TIMU YA TAIFA YA RWANDA AMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI ILIYOTOKEA MAENEO YA TAZARA JIJINI DAR ES SALAAM ALFAJIRI YA SAA 10 BAADA YA GARI ALILOKUWA NA WENZAKE KUTUMBUKIA MTARONI NA YEYE KUFARIKI PAPO HAPO.

BLOGU HII INAWAPA POLE WANACHAMA, WAPENZI, MASHABIKI, VIONGOZI WA SIMBA NA WANANCHI WA RWANDA PAMOJA NA WANAMICHEZO WOTE KWA MSIBA HUU MZITO.

Sunday, May 13, 2012

Tamati ya Ligi ya England


Mwali bado kafichwa kwa sababu mwenye dau kubwa bado hajajulikana, japokuwa ni kati ya wababe wawili wa Manchester - Manchester City na Manchester United.
Man.united ushindi 2009
Bingwa 2009 Man.United
Timu hizi mbili zina pointi 86, lakini City wana mabao mengi manane kuliko United.
Kwa kuzingatia hayo, mechi muhimu zaidi Jumapili hii ni ile inayozikutanisha Manchester City na Queen Park Rangers (QPR), mchezo unaofanyika Etihad, nyumbani kwa City mbele ya washabiki wake.
Mechi nyingine inayotia wadau matumbo joto ni ile ya Manchester United na Sunderland, United safari hii wakichezea ugenini.
Ili City watwae ubingwa wanatakiwa kuwa na matokeo kama ya United au mazuri zaidi. Kwa kifupi ni kwamba, City wakishinda kuna uwezekano mkubwa wa kutangazwa wafalme wa soka wa England.
Ferguson
Mazowea ya Ferguson kila mwaka
Ni katika hali hiyo Kocha Mkuu wa Manchester United, Sir Alex Ferguson anasema wao wanaombea litokee jambo la 'kijinga' dhidi ya jirani zao (Manchester City) ili wanyakue tonge mdomoni mwao. Kwamba wao United watatekeleza wajibu wao kujitahidi kushinda mechi yao, lakini kulipata kombe itategemea nyumba ya jirani.
Lakini ikumbukwe kwamba vijana hao wa Roberto Mancini katika msimu wote wamepoteza pointi mbili tu katika uwanja wao huo wa Etihad, yaani wameshinda mechi zote isipokuwa mbili tu walizotoka sare.
Ndiyo maana washabiki wao wengi wana matumaini makubwa ya kutwaa ubingwa walioupata mara ya mwisho mwaka 1968. Wanachotegemea dhidi ya QPR ni ushindi tu.
QPR wananolewa na kocha wa zamani wa City, Mark Hughes aliyetupiwa virago Desemba 2009 baada ya kushinda mechi mbili tu kati ya 11 City walizocheza mfululizo. Kocha huyo pia ameichezea United na Ferguson anamtegemea 'amsaidie kuiangamiza City'. Kwa ujumla timu mbili hizi za Manchester zinatarajiwa kuibuka na ushindi kwenye mechi zao hizi za mwisho.
Ligi ya Mabingwa Ulaya
Moja ya mambo yanayotafutwa kwenye mbio za Ligi Kuu ya Uingereza ni nafasi za timu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Kwa minajili ya Uingereza wakati huu, panaweza kuwapo nafasi moja au mbili, wakati timu zinazowania ni Arsenal wenye pointi 67,
Tottenham waliojikusantia pointi 66 na Newcastle waliovuna pointi 65.
Mechi muhimu katika kuamua hili ni kati ya Everton na Newcastle; Tottenham Hotspur dhidi ya Fulham na West Brom wanaoikaribisha Arsenal.
Hali ilivyo ni kwamba hatima ya Arsenal imo mikononi mwao wenyewe, kwa maana kwamba wanachotakiwa ni kushinda tu ili kufuzu moja kwa moja, bila kusubiri matokeo ya mechi nyingine. Ushindi utawahakikishia kubaki nafasi ya tatu wanayoshikilia
Hata hivyo, ikiwa Arsenal watatoa sare dhidi ya Baggies, wanaweza kuvukwa na kutupwa nafasi ya nne ikiwa Tottenham watawafunga Fulham.
Maana yake ni kwamba Washika Bunduki hao wa London hawatakuwa na chaguo zaidi ya kuingia kwenye mechi za mchujo ili kufuzu, huku Spurs wakisonga moja kwa moja kwenye mashindano hayo makubwa ya Ulaya.
Ikiwa Arsenal watachezea kichapo nyumbani kwa West Brom, ni dhahiri pia watakuwa wamejiweka pabaya, kwa sababu wataweza kupitwa na Spurs watakaohitaji sare tu
ikiwa Arsenal itafungwa mabao mawili au zaidi. Arsenal pia watapitwa na Newcastle inayonolewa na Alan Pardew, ikiwa watawafunga Everton.
Vinginevyo ni kwamba Tottenham wakishinda mechi yake tu itakuwa imejihakikishia kupata nafasi ya nne na sare pia inaweza kuitosheleza ikiwa Newcastle hawatawafunga Everton.
Kwa upande mwingine, ili Newcastle waweze kuingia kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, lazima wawafunge Everton na kuomba ama Arsenal au Tottenham wasishinde mechi zao. Ikiwa hizo tatu zitatokea, basi Newcastle itamaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu.
Hata hivyo, ikiwa Chelsea itatwaa Kombe la Mabingwa Ulaya kwenye fainali dhidi ya Bayern Munich mjini Munich Mei 19 mambo yatabadilika Uingereza, kwa sababu timu itakayoshika nafasi ya nne kwenye EPL mwaka huu haitakuwa na nafasi kwenye ligi hiyo tena.
Badala yake, timu hiyo itaingia kwenye Ligi ya Europa pamoja na watakaomaliza ligi wakiwa nafasi ya tano, kwani timu inayotwaa kombe hilo inashiriki msimu unaofuata kulitetea.
Katika mazingira haya, Arsenal watatakiwa kutumia vyema nguvu na fursa kuwamaliza West Brom, kwani kwao msimu ni kama umeshaisha tu, hawana kikubwa cha kupata wala kupoteza.
Spurs wanaelekea pia kwamba watawafunga Fulham, na maana ya haya ni kwamba kuna kila dalili za Newcastle kuachiwa simanzi bila kupenda.
Pengine Bayern watalitwaa kombe la Ligi ya Mabingwa, na kwa kufanya hivyo mazingira ya Ligi kuu ya England na ushiriki wa msimu ujao kimataifa kutoathiriwa.

Thursday, February 23, 2012

UWANJA WA NDEGE SONGWE MBEYA NI KITENDAWILI!!


Hili ni jengo la kupokelea abiria mpaka sasa uwanja huu haujulikani utakamilika lini kwani toka mwaka jana walisema mwezi wa kumi na mbili 12 utaanza kufanya kazi lakini mpaka sasa uwanja huo unaendelea kujengwa na haijulikani utakamilika lini.

Hii ni barabara ya kutua na kurukia ndege ikiwa imekamilika.
Hii ndiyo hali ya halisi ya uwanjani hapo kitendawili chake hatujui kitateguliwa lini.
CREDIT TO MBEYAYETU BLOG.

Airtel YakabidhiMilioni 50 Kwa Mshindi Wa Pili Wa MZUKA Promo!

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akikabidhi hundi ya
mfao ya shilingi milioni 5o/= kwa mshindi wa pili wa promosheni ya
Airtel MZUKA Bi Khadija Omari Issa (kushoto) wakati Afisa Mawasiliano
wa Airtel Bi Dangio Kaniki (shoto) akishudia. Makabidhiano hayo
yamefanyika katika ofisi kuu za Airtel jijini dar es salaam leo.
Mshindi wa pili wa promosheni ya Airtel MZUKA Bi Khadija Omari Issa
akionyesha cheki yake ya milioni 50/= zawadi alijishindia katika
promosheni kabambe ya Airtel MZUKA inayoendeshwa na Airtel mara baada
ya hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi kuu za
Airtel jijini dar es salaam leo.
Mshindi wa pili wa promosheni ya Airtel MZUKA Bi Khadija Omari Issa
akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani).
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiongea na
waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kukabidhi
zawadi ya shilingi milioni 50/= iliyofanyika ofisi za Airtel zilizopo
Morocco kwa mshindi wa promosheni ya Airtel MZUKA wakati kulia ni
Mshindi huyo Bi Khadija Omaria, wakwannza shoto ni Afisa Mawasiliano
wa Airtel Bi , Dangio Kaniki leo.
====
• Mshindi wa promo ya mwisho MZUKA kupatikana mwanzoni mwa Machi
• Promsheni mpya ya NANI MKALI itaendelea kufaidisha watea na
zaidi ya milioni 200.
Dar es Salaam 22/02/2012 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo
imekabidhi kitita cha shilingi milioni 50 kwa mshindi wake wa pili wa
promosheni yao kubwa ya MZUKA inayokaribia kuisha mwishoni mwa mwezi
huu.
Akiongea wakati wa makabidhiano hayo Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson
Mmbando alisema promosheni hii ni ya muda wa miezi mitatu na tuliahidi
kutoa zawadi zenye thamani ya thamani ya hadi milioni 600/= kwa hiyo
leo milioni hizi 50 zinazoenda kwa Bi Khadija Omari Issa Mkazi wa Dar
es Salaam eneo la Magomeni
Kitita hicho cha Airtel MZUKA shilingi milioni 50 tayari kimewekwa
katika akaunti yake na sasa anaweza kuzitumia kuanza kufanikisha
mipango na malengo yake aliyojiwekea
Pia kwa kupitia Promosheni hii ya MZUKA wa Airtel tayari tumesha toa
zawadi nyingine nyingi ikiwemo simu za Sumsung za kisasa zianzotumia
laini mbili zaidi ya 1,200 pia Sumsung Galaxy S2 zaidi ya 360 na vile
vile Sumsung Galaxy 7.0 zaidi ya 180 kwa wateja wetu mbalimbali
walioko nchini Tanzania.
Bado mteja wa Airtel unanafasi ya kujishindia zawadi zilizobaki
kupitia promosheni ya mzuka ikiwemo zawadi kubwa ya shilingi milioni
50 ambapo itatolewa kwa mteja mmoja tarehe 2 marchi 2012. Pia bado
zawadi nyingine za simu za Sumsung galaxy kila siku na kila wiki
zinaendelea kutoka kama kawaida
Ili mteja aweze kushinda ni rahisi na pia ni bure. Shiriki kwa kutuma
neno MZUKA kwenda 15565 na namba yako itakuwa inaingia kwenye droo
bure
Nae mshindi wa pili wa promosheni Bi Khadija Omari alisema “Naishukuru
sana Airtel kwa kuniwezesha kujipatia mamilioni haya ya fedha ambayo
msaada mkubwa sana kwangu ninawashauri wenzangu ambao hamjashinda
endeleeni kushiriki kwani mnaweza kuibuka washindi wa ili droo ya
mwisho inayofuata
“Nitaitumia zawadi yangu kuboresha maisha yangu ili niweze kutimiza
ndoto zangu nilizokuwa nazo tangu awali alimaliza kwa kusema Bi
Khadija
Artel Tanzania inaendesha na promosheni nyingine mpya ya NANI MKALI
ambapo zaidi ya milioni 200 zinashindaniwa, Ili kushiriki promosheni
hiyo mteja anatakiwa kutuma nene MKALI kwenda 15656 bure na kisha
ataanza kupokea maswali tofauti na kila atakapokuwa akijibu maswali
hayo kwa kujibu sms hizo atapata pointi na kujiongezea nafasi ya
kushinda.
Kila SMS itatozwa shilingi 350 tu hii ni pamoja na kodi. Promosheni
zote za Airtel zinadhamira ya kuwazawadia wateja wote wa Airtel ambao
wamekuwa wateja wazuri na kutumia huduma za Airtel kila siku.

Sunday, February 19, 2012

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar atembelea kijiji cha Mchekeni Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini kuwapa pole waliopatwa na janga la nyumba zao kuteketea kwa moto

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIZUNGUMZA NA BAADHI YA WAKAAZI WA MCHEKENI KIWENGWA AMBAO NYUMBA ZAO ZIMETEKETEA KWA MOTO.KUSHOTO YAKE NI MKUU WA WILAYA YA KASKAZINI B ND. VUAI ALI VUAI, KULIA YA BALOZI NI MKUU WA MKOA KASKAZINI UNGUJA MH. PEMBE JUMA KHAMIS NA PEMBENI NI BALOZI WA NYUMBA KUMI MCHEKENI ND. ELYAS YAQOUB.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIMKABIDHI SHILINGI LAKI NNE {400.000/- } SHEHA WA SHEHIA YA KIWENGWA BWANA MAULIDI MASOUD AME KWA AJILI YA KUWAFARIJI WANANCHI WA MCHEKENI AMBAO NYUMBA ZAO NANE ZIMETEKETEA KWA MOTO JUMAMOSI JIONI YA TEREHE 18/2/2012.
KATI KATI NI MKUU WA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA MH. PEMBA JUMA KHAMIS.
****

Ujeuri wa Chisora Waishia Ulingoni!!


Vitali Klitschko alifanikiwa kuhifadhi mkanda wake wa WBC uzani wa heavy mjini Munich, Ujerumani, licha ya kwamba mpinzani wake kutoka London, Dereck Chisora, alimtoa jasho hadi mwisho wa pigano hilo.
Chisora, ambaye amepungua kwa nchi sita akijilinganisha na kimo cha bondia huyo wa Ukraine, alionekana akiwa wa kwanza kushambulia katika kila raundi ya pigano hilo la raundi 12.
Klitschko, mwenye umri wa miaka 40, huenda sasa akataka kupigana tena na bingwa wa zamani kutoka Uingereza, David Haye.
Tangu kengele ya kwanza ilipolia, Chisora, ambaye ni mzaliwa Zimbabwe, alionyesha ukakamavu, akisonga mbele kumshambulia bingwa wa dunia na kujaribu kuvuruga mbinu za Klitschko za kujihami.
Lakini bingwa huyo wa dunia ambaye hajawahi kupigwa katika mapambano 44 ya kulipwa, alionyesha ni stadi mno kwa kukwepa makonde ya Chisora, na mara kwa mara akimwangushia ngumi kali za kichwa kwa mkono wa kulia.
Pigano hilo lilikwisha kwa mabondia hao wawili kujibizana kwa matusi, huku mdogo wake Klitschko, Wladimir Klitschko akisimama kati yao.
Ushindi huo bila shaka ni funzo kwa Chisora ambaye alimuonyesha Klitschko ujeuri hata kabla ya pambano, wakati alipomzaba kofi siku ya Ijumaa wakati mabondia hao wawili wakipimwa uzani mbele ya waandishi wa habari.
Frank Warren, ambaye anapanga mapambano ya Chisora, sasa amesema anamtaka Muingereza huyo aidha kupigana tena na Klitschko, au angalau mdogo wake, Wladimir.

Thursday, February 16, 2012

WADAU MSAADA UNAHITAJIKA WA SHILINGI MILIONI 45 BEATRICE ATIBIWE INDIA!!


Baetrice Emanuel Kantimbo
Baetrice Emanuel Kantimbo(48)mkazi wa kwembe kata ya Kibamba,jijini Dar es salaam anaomba msaada wa fedha za kumuwezesha kutibiwa mguu wake huko nchini India,kiasi cha milioni 45 zinahitajika.
Mguu huo una zaidi ya miaka 12 toka augue na hivi majuzi alifanyiwa upasuaji hospitali ya taifa muhimbili na kuondolewa nyama zilizooza.amepimwa hana kansa,kisukari wala shinikizo la damu.
Kwa mawasiliano zaidi +255716 850 350 au+255767 850 351 kwa m-pesa au tigo pesa.
CHANZO: BOFYA

MASHINDANO YA KUTAFUTA TIMU YA TAIFA YA MASUMBWI YAENDELEA


Bondia Fabian Gaudence (kushoto) akioneshana ufundi wa kutupa masumbwi na Idd Pialali wakati wa mashindano ya kuchagua mabondia watakaowakilisha taifa katika mashindano ya Kimataifa yanayotaraji kufanyika hivi karibuni. Gaudence alishinda kwa pointi. 

Mabondia Peter Stanley (kushoto) akipambana na Doto Shoka wakati wa mashindano ya kutafuta mabondia watakaoliwakilisha taifa katika mashindano ya Kimataifa.

TZ GOVERNMENT PRESENTS PAPER ON COMPREHENSIVE AFRICA AGRICULTURE DEVELOPMENT PROGRAMME.

Above and Below is Permanent Secretary Ministry of Agriculture Food Security and Cooperatives Mohamed Muya presenting  Tanzanian Country Paper on Comprehensive Africa Agriculture Development Programme (CAADP) / Grow Africa Partnership Implementation Status to the senior Officials consultative meeting held today in Dar es Salaam.
Above and Below some of the senior officials from different African Countries listening the key messages for aligning the proposal with CAADP frame works and Grow Africa Partnership Platform.

SHIRIKA LA SAVE THE CHILDREN LAZINDUA KAMPENI YA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO KWA WATOTO: MDAU WA HAKI ZA WATOTO HOYCE TEMU ASHAURI ELIMU YA LISHE ITOLEWE KWA WANANCHI.

 Baadhi ya Wanafunzi hao wakiwa na Mh. Hilda Ngowi.
 Mh. Mbunge wa Viti Maalum toka mkoa wa Iringa Lediana Ng'ong'o akizungumza na waandishi wa habari ambapo ametoa ushauri kwa  serikali kuwaajiri wataalam wa lishe kwa kila wilaya ili kufanikisha malengo ya Mkakati wa Kitaifa wa Lishe wa 2011/12 hadi 2015/16.
 Mwanaharakati wa Haki za Watoto na Afya zao Bi. Hoyce Temu akizungumza na wanahabari kuhusiana na kampeni ya kupambana na utapiamlo kwa watoto, ambapo amesema tatizo hilo ni kubwa sana hapa nchini na kuishauri serikali ielimisha jamii umuhimu wa kula chakula bora na pia kutoa ufafanuzi kuwa chakula bora ni kipi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
ASANTE SANA KWA KUTEMBELEA HAPA KARIBU TENA | KUSOMA HABARI ZILIZOPITA BOFYA OLDER POSTS