Searching...
Thursday, August 21, 2014

RASMI: MARCOS ROJO AMWAGA WINO MIAKA MITANO MANCHESTER UNITED

Rojo katua : Manchester United wamekamilisha usajili wa  Marcos Rojo kutoka Sporting Lisbon.

MANCHESTER United imethibitisha kumsajili beki wa Sporting Lisbon, Marcos Rojo kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 16.
Rojo, aliyewasili mjini Manchester siku ya jumanne jioni na kusema kujiunga na United "Anahisi kama ndoto' amesaini mkataba wa miaka mitano baada ya kufuzu vipimo vya afya na kukubaliana mambo binafsi.
Kipau mbele cha Louis van Gaal ilikuwa ni kusajili beki wa kushoto na aliamua kubadili mtazamo kwa kumsajili Rojo mwenye miaka 24 kufuatia kipigo cha jumamosi dhidi ya Swansea City.
Beki huyo raia wa Argentina atavaa jezi namba 5.
First team member: Rojo will wear the No 5 shirt and has signed a five-year contract at the club
Anaingia kikosi cha kwanza: Rojo atavaa jezi namba 5 na amesaini mkataba wa miaka mitano

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!