MWANASOKA
bora wa dunia, Cristiano Ronaldo jana ameungana na wachezaji wenzake wa
Real Madrid katika mazoezi ya kujiandaa na msimu nchini Marekani.
Ilikuwa
ni siku yake ya kwanza anafanya tena mazoezi na timu yake hiyo, baada
ya kufanya vibaya kwenye Kombe la Dunia akiwa na nchi yake, Ureno
iliyotolewa katika hatua ya makundi akiambulia kufunga bao moja tu.
Alilakiwa
na mamia ya mashabiki katika uwanja wao wa mazoezi mjini Los Angeles
kabla ya kwenda kufanya mazoezi mepesi peke yake, huku wenzake
wakiendelea na program kamili.
Amerudi: Cristiano Ronaldo amerudi mazoezini Real Madrid kujiandaa na msimu mpya
Ronaldo akikimbia peke yake kujiweka fiti
Fabio Coentrao na Sergio Ramos pamoja na wachezaji wengine wa Madrid wakijifua tofauti na Ronaldo
0 comments:
Post a Comment