Searching...
Wednesday, July 30, 2014

BABA YAKE TEVEZ AACHIWA BAADA YA SAA NANE ZA KUSHIKILIWA NA WATEKAJI

BABA wa mchezaji wa zamani wa Manchester United na Manchester City, Carlos Tevez aliyetekwa jana nchini Argentina, ameachiwa baada ya saa nane za kushikiliwa. 
La Nacion ya Argentina imeripoti kwamba Juan Carlos Cabrera alikuwa anaendesha gari lake katika Manispaa ya Moron, jimbo la Buenos Aires, wakati anatekwa asubuhi ya leo.
Klabu ya Tevez, Juventus ilithibitisha kumruhusu mshambuliaji huyo kwenda Argentina baada ya tukio hilo asubuhi ya jana.
Sasa shwari; Carlos Tevez alilazimika kurejea Argentina kumuokoa baba yake aliyetekwa
Carlos Tevez akiwa na baba yake, Juan Carlos Cabrera 

Gari aina ya Volkswagen Vento ilikutwa imetekelezwa na tovuti za  Argentina zikaripoti kwamba watekaji walikuwa wanataka fedha ili kumuachia. Hata hivyo, baada ya hapo suala hilo lilifanywa kuwa siri kwa matakwa ya familia ya Tevez.
Tevez alichukuliwa na shangazi yake mjamzito na mumewe, Segundo Tevez akiwa mdogo na kuanza kulelea tangu hapo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!