SHABIKI
wa Timu ya Yanga SC, Deodatus Isaya Lusinde, mkazi wa Kipunguni A,
amefariki dunia leo baada ya kuanguka ghafla wakati akishangilia bao la
Yanga lililofungwa na Didier Kavumbagu katika dakika ya 14 kipindi cha
kwanza.
Marehemu
amepoteza maisha akiwa chumba cha matibabu mara baada ya kuwekewa
mashine ya oksijeni na taarifa kuhusu kifo cha shabiki huyo
zimethibitishwa na mmoja wa madaktari aliyemhudumia akiwa uwanjani kabla
ya mauti kumfika, Nassor Matuzya.
Bwana Isaya alikuwa Meneja wa Bar ya Rose Hill iliyopo Segerea jijini
Dar. Ameacha mke aitwaye, Rose William Lusinde ambaye ni askari
magereza.
Marehemu amekutwa na mauti hayo wakati wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania
Bara, kati ya timu yake ya Yanga na Azam, mchezo uliomalizika kwa sare
ya bao 1-1.
Mungu ailaze roho ya mwanamichezo, Deodatus Isaya Lusinde mahali pema peponi. AMEN!
0 comments:
Post a Comment