Searching...
Saturday, February 11, 2012

Taswira Zaidi Za Mkutano Wa Sita Wa Bunge La Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania

Balozi Mulamula akiwa na afisa wa Bunge Bw. Prosper Minja kabla ya kuanza kwa kiako cha Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama.Balozi Mulamula (kulia) akijadili jambo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Edward Lowassa (Mb) mjini Dodoma leo. Balozi Mulamula alifika Dodoma kuhudhuria kikao cha Kamati hiyo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akiingia ndani ya ukumbi wa bunge leo mjini kuongoza kikao cha tisa cha mkutano wa sita wabunge ambapo bunge linahitimisha shughuli zake mjini Dodoma.

Mbunge wa Same Mashariki Anna Kilango akijadili jambo na Mwanasheria mkuu wa serikali Jaji Frederick Werema ndani ya ukumbi wa Bunge leo wakati wa kipindi cha maswali na majibu mjini Dodoma
Mbunge wa Singida mjini Mohammed Dewji akimsikiliza kwa makini Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu Stephen Wasira ndani ya ukumbi wa bunge leo mjini Dodoma.
Katibu Mtendaji wa jumuiya ya nchi za Maziwa Makuu aliyemaliza muda wake Balozi Liberata Mulamula (kulia) akisalimiana na kubadilishana mawazo na Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda Bungeni Dodoma leo.
Spika Makinda akifurahia jambo na Mbunge wa Simanjoro Mhe. Ole Sendeka (kati) na mdau wa michezo nchini,Wakili Imani Madega.
Balozi Mulamula (kulia) akisalimiana na Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah (kushoto) leo katika viwanja vya Bunge Dodoma leo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akifurahia jambo na wanafunzi wa shule ya sekondari Hijra ya mjini Dodoma nje ya ukumbi wa Bunge Dodoma.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akiwasalimia viongozi na wachezaji wa timu ya Villa Squard ya Kinondoni jijini Dar es salaam waliofika bungeni hapo kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na bunge.
Wajumbe na Viongozi wa chama cha wamiliki wa shule Vyuo na shule binafsi (TAMONGSCO) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoka ndani ya ukumbi wa bunge leo mjini Dodoma. Viongozi hao wapo bungeni Dodoma kukutana na kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za jamii kwa lengo la kuhimiza ushirikiano kati yao na wabunge pamoja na serikali ili kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazoikabili sekta binafsi ya elimu nchini Tanzania.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!