Searching...
Saturday, February 11, 2012

Hali Sasa ni Shwari Hospitali ya Taifa Muhimbili,Madaktari wote wanza kufanya kazi kama ilivyokuwa hapo awali


Baadhi ya Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimuhudumia mmoja wa wagonjwa waliokuwa wamelazwa katika wadi namba sita kwenye Jengo la Mwaisela kwenye hospitali hiyo.Madaktari hao ambao walikuwa kwenye mgomo kwa kipindi cha wiki mbili mfululizo,leo wameanza tena kazi mara baada ya kukutana na Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda jana na kuzungumza nae na kuafikiana kutekelezewa yale waliyoyahitaji.
Madaktari wa Muhimbili wakimfanyia matibabu mmoja wa wagonjwa waliolazwa kwenye hospitali hiyo leo.
Baadhi ya Wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakiwa wamekaa nje ya eneo ya huduma ya matibabu ya haraka wakisubiria wagonjwa wanaoletwa hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu.
Wauguzi wa Muhimbili wakimtoa mgonjwa MOI na kupempeleka kwenye wadi iliopo kwenye jengo la Mwaisela.
Mgonjwa alipokelewa na wauguzi wa kitengo cha Huduma ya Haraka kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili leo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!