Searching...
Thursday, July 7, 2011

Nchi za Afrika zapiga hatua kwenye masuala ya elimu

Waziri wa Elimu nchini Kenya Prof Sam Ongeri
Kutafuta njia za kumhakikishia kila mmoja elimu ndiyo ajenda kuu inayozungumziwa kwenye mkutano wa baraza la kiuchumi na kijamii la UM unaondelea mjini Geneva. Zaidi ya wajumbe 500 wanaowakilisha serikali , wafadhili , mashirika ya umma, sekta za kibinafsi na wasomi watajadili na kutoa mapendekezo jinsi dunia wakati huu wa hali mbaya ya uchumi inaweza kutimiza lengo la elimu kwa wote na kuhakikisha malengo ya milenia yametimizwa.
Akiongea kwenye mkutano unaozungumzia changamoto za elimu zinazolikumba bara la Afrika waziri wa elimu nchini Kenya Prof  Sam Ongeri amesema kuwa Afrika imeonyesha kupiga hatua kwenye masuala ya elimu tangu mwaka 2000 lakini  akasema kuwa kuna changamoto za kupata viwango vinavyohitajika vya elimu.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!