Searching...
Tuesday, May 10, 2011

Ubingwa wanukia Man United

Manchester United inahitaji pointi moja kutangazwa bingwa wa ligi kuu ya England, baada ya kushinda mchezo wake dhidi ya Chelsea kwa mabao 2-1.
Chelsea
Man U ikicheza na Chelsea
Magoli ya Havier Hernandez katika dakika ya kwanza na bao la kichwa la Nemanja Vidic yaliipa ushindi muhimu kwa Manchester United kusogelea ubingwa.
Goli pekee la Chelsea lilifungwa na Frank Lampard.
United walitawala zaidi kipindi cha kwanza, huku Chelsea wakipigana kufa na kupona katika kipindi cha pili.
Man United itakutana na Blackburn Jumamosi ijayo.

Arsenal yafungwa

Stoke
Mashabiki wa Stoke
Katika michezo mingine Arsenal imefungwa mabao 3-1 na Stoke City na kuthibitisha Arsenal kumaliza msimu bila ya kombe lolote.
Baada ya kuichapa Man U, Arsenal walikuwa na ari kubwa ya kushinda mechi zote zilizosalia, lakini walishindwa kutamba mbele ya Stoke.
Kenwyne Jones aliandika bao la kwanza la Stoke, huku Jermaine Pennant akipachika la pili na la tatu kufungwa na Jonathan Walters.
Bao pekee la Arsenal lilifungwa na Robin Van Persie.
Huko mkiani katika ligi kuu Wolverhampton imejisogeza hadi nafasi ya 17 baada ya kupata ushindi wa 3-1 dhidi ya West Brom.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!