
Ripoti hiyo imetoa mapendekezo kuhusu mwelekeo wa nchi za Afrika katika pande nne, kwanzi ni lazima kuwa na bidhaa na masoko ya aina mbalimbali; pili, kueneza elimu ya hali ya juu, na kuinua usimamizi wa uwezo wa kiteknolojia, tatu, kuwasaidia wanawake kuanzisha shughuli zao ili kujiendeleza; na nne kuendeleza uchumi wa utalii.
Katika ufunguzi wa mkutano wa Afrika wa Baraza la Uchumi wa Dunia Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alisema, nchi za Afrika zinapaswa kuzibadilisha nguvu zao za maliasili kuwa uwezo wa kujipatia maendeleo endelevu, na kuanzisha uhusiano wa ushirikiano wa aina mpya wakati zinapokuwa na mawasiliano ya kiuchumi na kibiashara na nchi na sehemu nyingine duniani, ili kutimiza lengo la kunufaishana.
0 comments:
Post a Comment