Searching...
Monday, April 25, 2011

Arsenal yaboronga

Matumaini ya Arsenal kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England yamefifia zaidi baada ya kufungwa 2-1 na Bolton.
Bolton
Bolton
Arsenal wakicheza chini ya kiwango chao katika kipindi cha kwanza walifungwa na Daniel Sturridge kwa bao la kichwa kufuatia mpira wa kona.
Mapema katika kipindi cha pili, Kipa Wojciech Szczesny aliokoa mkwaju wa penati uliopigwa na Kevin Davies, na dakika moja baadaye Robin Van Persie kufunga bao la kusawazisha kwa Arsenal.
Arsenal walikuwa na nafasi za kutosha kushinda mchezo huo, lakini walijikuta wakipoteza katika dakika ya mwisho.
Tamir Cohen aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona na kuwapa ushindi Bolton.
Arsenal walitakiwa kupata ushindi katika mchezo huu ili kuwa na matumaini ya kuwania ubingwa.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!