Searching...
Monday, April 25, 2011

Polisi Uchina wawatia waumini kizuizini

Polisi wa Uchina wamewatia kizuizini wafuasi wa kanisa liliopigwa marufuku la Shouwang.
Pasaka
Pasaka
Watu hao wasiopungua 20 walikamatwa walipokuwa wakifanya mhadhara wa pasaka wakiwa nje.
Kanisa hilo la ki-evangelisti lina wafuasi takriban elfu moja katika mji mkuu wa Beijing.
Viongozi kutoka kanisa hilo wamepewa kifungo cha nyumbani, na wafuasi wa kanisa hilo pia wamekuwa wakikamatwa katika majuma ya hivi karibuni, katika juhudi za serikali kuangamiza upinzani.
Katiba ya Uchina inawapa watu uhuru wa kufanya ibada,lakini Wakristo takriban 70,000,000 ni wafuasi wa makanisa yaliyopigwa marufuku.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!