Afrika Kusini imeadhimisha miaka 17 ya uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia ulioondoa sera ya ubaguzi wa rangi. Katibu mkuu wa chama ANC Bw. Gwede Mantashe amesema ANC haifurahishwi na hali ya wazungu nchini humo kumiliki asilimia 87 ya ardhi na asilimia 72 ya nyadhifa katika sekta za biashara na viwanda, pia aliishutumu kundi la Afrikaanerbond lililokuwa mhimili wa serikali ya kibaguzi kwa kutaka kuendeleza sera hiyo, akijibu malalamiko ya kundi hilo dhidi ya serikali ya Afrika Kusini kwamba inapuuza katiba na kutumia ovyo madaraka ya watu wengi
0 comments:
Post a Comment