Manchester United imepenya kuingia robo fainali ya kombe la FA baada ya kuifunga timu ya daraja la chini, Crawley Town kwa goli 1-0.
Crawley waliipa United wakati mgumu, na hata kufikia kugonga nguzo ya juu katika dakika za majeruhi kupitia mchezaji Richard Brodie.
Kipindi cha pili licha ya United kumchezesha Wayne Rooney, Crawley Town ilitawala mchezo, lakini haikuweza kufanikiwa kupata goli.
Katika michezo mingine Birmingham City imeinyuka Sheffield Wednesday mabao 3-0, na Stoke City kuichapa Brighton 3-0.
0 comments:
Post a Comment