Searching...
Monday, February 21, 2011

United yapenya Kombe la FA

Manchester United imepenya kuingia robo fainali ya kombe la FA baada ya kuifunga timu ya daraja la chini, Crawley Town kwa goli 1-0.
Town
Crawley Town FC
Goli hilo pekee la United limefungwa na Wes Brown katika dakika ya 28.
Crawley waliipa United wakati mgumu, na hata kufikia kugonga nguzo ya juu katika dakika za majeruhi kupitia mchezaji Richard Brodie.
Brown
Nahodha Wes Brown alifunga bao pekee na la ushindi
Manchester walionekana kupwaya katika safu ya ushambuliaji iliyokuwa na Bebe na Gabriel Obertan na Xavier Hernandez.
Kipindi cha pili licha ya United kumchezesha Wayne Rooney, Crawley Town ilitawala mchezo, lakini haikuweza kufanikiwa kupata goli.
Katika michezo mingine Birmingham City imeinyuka Sheffield Wednesday mabao 3-0, na Stoke City kuichapa Brighton 3-0.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!