Tangazo rasmi limetolewa kuthibitisha kuwa Rais Museveni ndiye mshindi katika uchaguzi uliofanywa Ijumaa.

Rais Yoweri Museveni
Bw Besigye amekataa kukubali matokeo hayo na kudai kuwa kulikuwa na udanganyifu katika shughuli ya uchaguzi.
Chama kilicho madarakani kimetuhumiwa kwa kutumia rasilmali ya serikali kuwahonga wapigaji kura.
Uchaguzi huo uliendelea kwa utulivu ingawaje kuna ripoti za vurugu kadhaa baina ya wafuasi wa chama kinachotawala na chama cha upinzani.
0 comments:
Post a Comment