Bingwa mtetezi Chelsea imetolewa katika raundi ya nne ya michuano ya kombe la FA, baada ya kufungwa na Everton kupitia mikwaju ya Penati.
Chelsea wakicheza nyumbani walipata bao la kuongoza katika dakika ya 104 lililofungwa na Frank Lampard, lakini Leighton Baines alisawazisha bao hilo dakika moja kabla ya kupenga cha mwisho kupulizwa na kulazimika kupigwa penati.
Phil Neville ndio alipiga mkwaju wa ushindi wa Everton.
Everton sasa itakutana na Reading katika raundi ya tano.
0 comments:
Post a Comment