Searching...
Monday, December 13, 2010

Mkataba ya kibiashara kati ya India na Jumuiya ya Ulaya kuathiri upatikanaji wa madawa:UM

Mjumbe maluum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya kuwa na afya nzuri Anand Grover amesema ameonya kuwa makubalino ya kibiashara kati ya India na Jumuiya ya ulaya huenda ikazuia mamilioni ya watu kupata madawa yanayookoa au kurefusha maisha.
Kwa sasa India ndiyo muuzaji mkubwa zaidi wa madawa kwenda kwa mataifa yanayoendelea lakini mkataba huo wa kibiashara unaojadiliwa kwa sasa kati ya India na Jumuiya ya Ulaya unahataraisha kutengenezwa kwa madawa hayo. Grover amesema kuwa mamilioni ya watu katika nchi zinazoendelea wanaitegemea India kwa madawa kwa bei nafuu na kuongeza kuwa kuzuia kuundwa kwa madawa hayo kutakuwa na madhara makubwa ya kiafya kote duniani. George njogopa na taarifa kamili

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!