Searching...
Monday, November 8, 2010

Polio yaripotiwa kuzuka DR Congo:WHO

Mkurupuko wa ugonjwa wa Polio umeripotiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku visa ya maambukizi 120 na vifo 58 vikiripotiwa.
Chanjo ya polio Afrika
Chanjo ya polio Afrika
Nusu ya visa vya ugonjwa huo vimeripotiwa kwa muda wa siku kumi zilizopita. Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa serikali ya DRC imeuatadharisha umma kuhusu ugonjwa huo na kuazisha shughuli za dharura kwa usaidizi wa mashirika ya WHO , UNICEF na US CDC huku kukitarajiwa kampeni tatu za kutoa chanjo kote nchini. Oliver Rosenbauer ni afisa wa WHO

WHO linasema kuwa ni muhimu kwa nchi zilizo kwenye kanda ya Afrika ya kati na pembe ya Afrika kuwa macho ili kuweza kutambua dalili zozote za ugonjwa huo . Limeongeza kuwa wasafiri kwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo watahitaji kuchanjwa dhidi ya ugonjwa huo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!