Searching...
Tuesday, June 15, 2010

Mji wa Barcelona nao kupiga marufuku vazi la wanawake wa Kiislamu la niqab

Sample ImageMji wa Barcelona wa nchini Uhispania unaonekana utajiunga na baadhi ya miji ya nchi za Ulaya iliyopiga marufuku vazi la niqab na burqa katika majengo ya serikali na tayari wanaharakati wa haki za binaadamu wamejipanga kukabiliana kisheria na jambo hilo.
Tayari miji mingine mitatu ya Uhispania ya Catalonia, El Venrell na Lerida imeshachukua uamuzi kama huo wa kuwapiga marufuku wanawake wa Kiislamu kuvaa mavazi hayo.
Hata hivyo hatua hizo zinalalamikiwa vikali na mashirika ya haki za binaadamu barani Ulaya yakisisitiza kuwa, kufanya hivyo ni kukanyaga haki na uhuru wa watu kuvaa mavazi wanayopenda.
Licha ya kudai kustaarabika na kuwa na demokrasia, lakini nchi za Ulaya ziko tayari kuvumilia wanawake kutembea nusu uchi katika mitaa ya miji ya nchi hizo kuliko kuruhusu wanawake kujisitiri vizuri.
Miongoni mwa nchi za Ulaya zilizowahi kuchukua hatua kama hizo ni Ufaransa na Ubelgiji.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!