Searching...
Wednesday, May 26, 2010

Viongozi wa Afrika watakiwa kugawa rasilimali za nchi kwa uadilifu

Sample ImageKamati ya watu mashuhuri wanaofuatilia maendeleo ya bara la Afrika imewataka viongozi wa Kiafrika kusambaza raslimali za nchi zao kwa uadilifu ili bara hilo liweze kufikia kilele cha saada na ufanisi. Kamati hiyo inayoongozwa na Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan imesema kwenye ripoti yake ya kila mwaka kuwa, ufisadi na uongozi mbaya ni miongoni mwa sababu zinazochangia bara la Afrika kubaki nyuma kimaendeleo. Akizungumza wakati wa kutolewa ripoti hiyo mjini Johannesburg Afrika Kusini, Kofi Annan amesema kuwa baadhi ya viongozi hawataki raslimali za nchi ziwafikie watu maskini na kutokana na hali hiyo umasikini umeendelea kulisakama bara hilo miaka nenda miaka rudi. Amewasihi viongozi waongozwe na uwazi na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao kwa raia.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!