Searching...
Thursday, May 27, 2010

Nairobi-Uharamia wa Somalia waleta hasara kubwa ya kiuchumi kwa nchi za Afrika Mashariki

Shirikisho la mawakala wa meli la Kenya limesema, kutokana na kupamba moto kwa utekaji nyara unaofanywa na maharamia wa Somalia, nchi za Afrika Mashariki zinapata hasara ya dola za kimarekani milioni 275 kwa mwaka.

Ofisa wa shirikisho hilo Bw. David Machay siku hiyo amesema, uchumi wa nchi mbalimbali za Afrika Mashariki zikiwemo Kenya, Tanzania na Uganda umeathirika vibaya kutokana na shughuli za uharamia. Aidha malipo ya bima ya meli yanaongezeka, na gharama za usafirishaji kwa njia ya meli pia zimepanda kutokana na makampuni ya meli kukodi meli za kufanya ulinzi.

Bw. Mackay alisema endapo jumuiya ya kimataifa haitachukua hatua za kuzuia na kupambana na uharamia nchini Somalia, mchakato wa kuendeleza viwanda katika nchi za Afrika Mashariki utaathiriwa vibaya.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!