Searching...
Friday, May 28, 2010

Wafanyakazi Afrika Kusini watishia kugoma wakati wa kombe la dunia

Sample ImageMuungano wa vyama vya wafanyakazi nchini Afrika Kusini COSATU umetishia kuitisha mgomo wa nchi nzima wakati wa mashindani ya kombe la dunia katika mchezo wa soka yanayotarajiwa kuanza Juni 10. Katibu Mkuu wa COSATU Nzwelinzima Vavi amesema kuwa mgomo huo huenda ukafanyika kutokana na kupanda bei ya umeme kiasi kwamba wananchi wa kawaida hawawezi kumudu gharama yake. Vavi amesema kuwa mkutano kati ya muungano huo na baraza la kushughulikia uchumi na maendeleo utafanyika Juni 14 na iwapo hakutopatikana natija yoyote kwenye mkutano huo basi mgomo huo utafanyika. Afrika Kusini itakuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuaanda dimba la kombe la dunia katika mchezo wa soka.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!