Searching...
Sunday, September 28, 2014

MAZEMBE YATOLEWA KWA MABAO YA UGENINI, FAINALI NI AS VITA NA SETIF LIGI YA MABINGWA

NDOTO za TP Mazembe kwenda Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hii leo zimeota mbawa baada ya kutolewa na ES Setif ya Algeria kwa mabao ya ugenini kufuatia sare ya jumla ya 4-4.
Setif walishinda 2-1 Algeria wiki iliyopita na leo, Mazembe wameshinda 3-2 mjini Lubumbashi- maaba yake timu ya Algeria inakwenda kuumana na AS Vita ra DRC pia mwezi ujao.
Mabao ya Mazembe leo yamefungwa na Mghana, Daniel Adjei Nii dakika ya 21, Salif Coulibaly wa Mali dakika ya 38 na Jonathan Bolingi dakika ya 53, wakati ya Setif yamefungwa na Abdelmalek Ziaya dakika ya tisa Sofiane Younes dakika ya 75.
Poleni vijana, haikuwa bahati yenu; Watanzania wanaochezea TP Mazembe, Mbwana Samatta kushoto na Thomas Ulimwengu kulia

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!