Searching...
Sunday, September 28, 2014

ALONSO AWAFUNGA WATU MIDOMO BUNDESLIGA, APIGA PASI 175 MECHI MOJA


Wakati Xabi Alonso alipotua Bayern Munich, wengi walilalamika kwamba hakukuwa na haja ya timu hiyo kumchukua mkongwe huyo kuziba pendo la Toni Kroos aliyekwenda Real Madrid.

Badala yake wakasisitiza wangeweza kuwapa nafasi vijana.
Lakini kadiri siku zinavyosonga mbele, Xabi Alonso amezidi kutoa somo kwa kufanikiwa kuwa mchezaji bora wa mechi mara mbili katika mechi tano.
Kama hiyo haitoshi, Alonso amefanikiwa kugusa mpira mara 679, huku akipiga pasi 558 zilizofika ukiwa ni wastani wa  89% ambao ni wa juu kabisa.

Katika mechi wakati Bayern ilipoivaa Cologne jana, Alonso alipiga pasi 175, si mchezo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!