KOCHA
Arsene Wenger amempa jezi namba 23 mshambuliaji mpya alyemsajili kwa
Pauni Milioni 16kutoka Manchester United, Danny Welbeck.
Welbeck,
ameamua kuondoka Old Trafford baada ya kuona hana nafasi kwenye kikosi
cha kwanza cha kocha Mholanzi, Louis van Gaal na alilazimisja uhamisho
wa moja kwa moja baada ya awali, United kutaka kumtoa kwa mkopo wa Pauni
Milioni 3 Arsenal.
Welbeck
anakwenda kuanza maisha mapya The Gunners baada ya kusaini Mkataba wa
miaka mitano akiwa na matumaini makubwa ya kung'ara kutokana na
mapungufu ya washambuliaji Arsenal.
Namba
ya jezi: Welbeck amechukua jezi namba 23, ambayo ilipatiwa umaarufu na
mcheza mpira wa kikapu Michael Jordan na baadaye kiungo David Beckham
0 comments:
Post a Comment