KLABU ya QPR imeimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa kumsajili mshambuliaji wa Napoli, Eduardo Vargas kwa mkopo wa muda mrefu.
Habari hizi ni njema kwa kocha Harry Redknapp ambaye alikuwa ana washambuliaji watatu tu kikosini kabla ya uhamisho huu.
Mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 24 mzunguko wa pili wa msimu uliopita
alicheza kwa mkopo La Liga katika klabu ya Valencia, ambako alifunga
mabao matano katika mechi 25.
0 comments:
Post a Comment