Kijana mpya: Liverpool wametangaza rasmi kumsajili beki wa kushoto wa Hispania Alberton Moreno.
BEKI wa pembeni wa Hispania, Alberto Moreno amesajiliwa na Liverpool kwa dau la paundi milioni 12.
Makubaliano yalifikiwa mapema wiki hii, lakini klabu imetangaza rasmi mwishoni wa wiki hii.
Kinda huyo mwenye miaka 22 anafurahia
mafanikio yake ndani ya miaka miwili iliyopita akiwa ametwaa ubingwa wa
mataifa ya Ulaya akiwa na timu ya taifa ya Hispania chini ya miaka 21
mwaka 2013 na baadaye aliingia kikosi cha kwanza cha klabu ya Sevilla.
Moreno alishinda ligi ya Europa msimu
uliopita akiwa na Sevilla na alitoa machozi baada ya kupigwa mabao 2-0
na Real Madrid katika mechi ya fainali ya 'UEFA Super Cup' siku ya
jumanne.


0 comments:
Post a Comment