MWANASOKA
bora wa dunia, Cristiano Ronaldo aliishuhudia timu yake Real Madrid
ikifungwa 1-0 na Roma akiwa bench katika mchezo wa mwisho wa kujiandaa
na msimu mpya usiku wa kuamkia leo nchini Marekani.
Bao
pekee la Francesco Totti dakika ya 58 mjini Texas lilitosha kuiangusha
timu ya Carlo Ancelotti ambayo ilicheza bila mshambuliaji.
Mechi
hiyo ilikumbwa na vitimbi mwishoni baada ya mashabiki kuvamia uwanja
kwenda kuwakumbatia na kupiga nao picha wachezaji wawapendao.
Benchi: Cristiano Ronaldo alikuwa benchi Real Madrid ikimenyana na Roma
Winga wa Real, Gareth Bale akitafuta mbinu za kumpokonya mpira mpinzani
Shabiki akijipiga picha na nyota wa Real Madrid, Isco
Polisi akimdhibiti mmoja wa mashabiki waliovamia uwanja
Francesco Totti akifunga bao pekee la ushindi
0 comments:
Post a Comment