Searching...
Wednesday, July 23, 2014

MAAMUZI YA PATRICK VIEIRA KUITOA MAN CITY UWANJANI BAADA YA FOFANA KUBAGULIWA, YAUNGWA MKONO NA MANUEL PELLEGRINI

Flashpoint: Seko Fofana (No 8) kicked out at a NHK Rijeka player after being allegedly racially abused
Seko Fofana (Jezi namba 8) alimpiga mchezaji wa kNHK Rijeka baada ya kubaguliwa.

Imechapishwa Julai 23, 2014, saa 6:32 mchana

Patrick Vieira alikuwa sahihi kukitoa nje ya uwanja kikosi cha wachezaji wa timu ya vijana ya Manchester City  baada ya wanandinga wake kuoneshwa vitendo vya ubaguzi wa rangi, amesema kocha Manuel Pellegrini.
Vieira alisimamisha mechi dhidi ya NHK Rijeka katika ziara yao nchini Croatia kujiandaa na msimu mpya baada ya kinda mwenye miaka 19, Mfaransa, Seko Fofana kubaguliwa.  
Pellegrini alisema: 'Sijui sana kuhusu hilo, lakini kama Patrick aliona ni sahihi kuwatoa uwanjani wachezaji, basi itakuwa kitu sahihi'.
Seeing red: Fofana was sent off for kicking out at his opponent as the players come together
Kadi nyekundu: Fofana alioneshwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mpinzani wake
Taking a stand: Patrick Vieira (third left) walked onto the pitch after hearing what may have happened
Alionesha msimamo: Patrick Vieira (wa tatu kushoto) akiingia uwanjani baada ya kusikia kilichotokea.
Stopped: The match is abandoned as Vieira leads his team off the pitch in Croatia
Ngoma imeisha: Mechi iliahirishwa baada ya  Vieira kuwaongoza wachezaji wake kutoka nje ya uwanja nchini   Croatia
'Alitathimini hali halisi na alifanya kitu sahihi. Haiwezekani kuendelea kucheza wakati kitu kama hiki kimetokea'.
Fofana alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mpinzani wake, lakini klabu imeeleza imani yake kuwa Fofana, kijana mwenye kipaji kikubwa, alibaguliwa kabla ya kutokea kwa tukio hilo. Tukio hilo lilitokea kabla ya mapumziko.
Maamuzi ya kuahirisha mechi yalichukuliwa na viongozi waliokuwa na kikosi hicho  na Vieira aliamua kumuunga mkono kinda huyo kwasababu alikuwa na mawazo mengi kutokana na tukio hilo.
Taarifa ya klabu jana jioni ilisomeka: 'Kikosi cha vijana chini ya miaka 20 cha Manchester City kilikuwa na mchezo dhidi ya  HNK Rijeka leo (jumanne) na imeahirishwa kutokana na tukio la kiungo kijana,  Seko Fofana  kubaguliwa na mchezaji wa timu pinzani'.
Youngster: Fofana in action during an Under-21 match against Chelsea last season
Kinda: Fofana akiwa akionesha vitu vyake katika mechi dhidi ya  Chelsea ya vijana chini ya miaka 21 msimu uliopita.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!