Searching...
Sunday, July 20, 2014

JESHI MISRI LAMUONDOA MOHAMED SALAH CHELSEA

MUSTAKABALI wa Mohamed Salah katika klabu ya Chelsea upo shakani, baada ya kutakiwa kurejea nyumbani kwao, Msiri kuchukua mafunzo ya jeshi.
Salah, aliyehamia Stamford Bridge kutoka Basle ya Uswisi Januari mwaka huu, ameruhusiwa kuishi England kwa kigezo cha kushiriki masomo.
Pamoja na hayo, usajili wake umesitishwa na Wizara ya Elimu ya Juu Misri, tovuti ya soika ya www.kingfut.com imesema, maana yake mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anaweza kurudi nchini mwao.

Jeshini kwanza; Mo Salah anatakiwa kurudi nyumbani kupata mafunzo ya Jeshi

Ikiwa Salah, aliyeichezea Chelsea mchezo wa kirafiki dhidi ya AFC Wimbledon jana atatakiwa kurejea nyumbani, hataruhusiwa kuondoka tena Misri hadi akamilishe mafunzo ya kijeshi, yanayochukua mwaka mmoja hadi mitatu.
"Salah ameelesea namna alivyoshitushwa juu ya uamuzi huu," amesema Mkurugenzi wa timu ya taifa ya Misri, Ahmed Hassan.
"Ameniambia anajaribu kuiwakilisha Misri katika njia nzuri zinazowezekana. Na haya ndiyo matokeo yake kutoka kwa nchi yake?'
Kikao kinatarajiwa kufanyika baina ya FA ya Misri, benchi la ufundi la timu ya taifa na Waziri wa Elimu ya Juu, kutafuta suluhisho.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!