Searching...
Wednesday, July 23, 2014

DUNGA KOCHA MPYA BRAZIL, ASEMA AMEFURAHI ILE MBAYA

SHIRIKISHO la Soka Brazil (CBC) limeteua Dunga kuwa kocha mpya wa timu ya taifa leo, wiki mbili baada ya kipigo cha ainu cha mabao 7-1 kutoka kwa Ujerumani kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Dunia, kilichomfanya kocha Luiz Felipe Scolari abwage manyanga.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 50, aliyekuwa nahodha wa kikosi cha Brazil kilichotwaa Kombe la nne la Dunia mwaka 1994, mara ya mwisho alikuwa kocha wa timu hiyo mwaka 2010 alipofukuzwa baada ya timu kutolewa katika Robo Fainali ya Kombe la Dunia Afrika Kusini.
"Nina furaha kurejea,"aliwaambia Waandishi wa Habari.

Dunga amerejeshwa kuinoa Brazil baada ya kuboronga Kombe la Dunia chini ya Scolari 
Headache: Scolari resigned after the World Cup where Brazil were thrashed 7-1 by Germany in the semis
Scolari alijiuzulu baada ya Brazil kufungwa 7-1 na Ujerumani Kombe la Dunia

Aliiongoza Brazil hadi Robo Fainali ilipotolewa kwa kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Uholanzi, lakini akalaumiwa kwa mbinu zake mbovu na kufukuzwa na nafasi yake kuchukua Mano Menezes.
Awali aliiwezesha timu hiyo kushinda mechi 42, ndani take akitwaa mataji ya Copa America mwaka 2007 na Kombe la Mabara mwaka 2009, akipoteza mechi sita tu kati 60. 

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!