AS Roma imeendelea vyema katika mbio za ubingwa baada ya kuilaza AC Milan mabao 2-0 jana.
Shukrani
kwao wafungaji wa mabao hayo, Miralem Pjanic na Gervinho siku ambayo
mshambuliaji wa AC Milan, Mario Balotelli alimuwakia kocha wake,
Clarence Seedorf kwa kumtoa nje.
Matokeo
hayo yanapunguza pengo la pointi kati ya Roma inayoshika nafasi ya pili
na Juventus iliyo kileleni hadi kubaki pointi tano kabla ya vinara hao
wa Serie A kucheza na Sassuolo Jumatatu.
0 comments:
Post a Comment