ZIKIWA
zimebaki saa chache kushuhudia timu itakayoungana na Real Madrid katika
mchezo wa fainali ya UEFA mei 24 mjini Lisbon nchini Ureno kati ya
Chelsea au Atletico, Jose Mourinho ametetea mbinu yake ya kupaki basi
inayolalamikiwa na makocha wengi.
Mourinho amesema kuwa kuna
falsafa nyingi za soka na anashangaa wanaolalamika juu ya mbinu zake
kwasababu asingefanya hivyo angekuwa anafungwa mara nyingi.
Kocha huyo raia wa Ureno
alilalamikiwa `kupaki basi` na Atletico Madrid kwenye uwanja wa Vicente
Calderon na kulazimisha suluhu ya bila kufungana.
Jumapili iliyopita, alitumia
mbinu kama hiyo na kuwafunga Liverpool mabao 2-0 uwanja wa Anfield na
kufufua matumaini kidogo ya kutwaa ubingwa, lakini kocha wa majogoo wa
jiji Brendan Rodgers alimlalamikia Mourinho kwa kupaki basi na kusema
anacheza mpira wa kizamani.
Japokuwa wengi wanalalamika kuwa
Chelsea wanatumia mbinu za zamani nje ya mpira wa kisasa, Mreno huyo
amewashangaa na kusema kikosi chake kina nguvu na kucheza mpira safi.
Mourinho katika mkutano na
waandishi wa habari amesema: “Unajua, siku hizi kuna wataalumu wengi wa
soka na wanafahamu zaidi mpira kuliko mimi, wana mitazamo ya juu, hakika
inastaajabisha”.
“Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli: kama timu haijilinda vizuri na kufunga mabao mengi, basi kutakuwa na tatizo kubwa”.
“Timu bila usawa sio timu.
Mpinzani anapokuwa na mpira lazima ujitahidi kumzuia asikufunge.
Tunapokuwa na mpira tunajaribu kufunga. Huo ndio mpira-mpira ninaoujua”.
“Nakumbuka nilisema mara ya
kwanza nilipofika hapa, kama una kipa kama Petr Cech anayeweza kupiga
mpira mpaka kwenye boksi la mpinzani , halafu kuna mshambuliaji kama
Didier Drogba anayejaribu kila mpira wa juu, kwanini ucheze mipira
mifupi? Ukifanya hivyo labda ni mpumbavu”.
0 comments:
Post a Comment