Searching...
Wednesday, May 15, 2013

LINDI MKOA UNAOHITAJI JICHO LA ZIADA KATIKA MIUNDOMBINU

 Mnara maalum ambao unautambulisha mkoa wa Lindi.

Camera ya Father Kidevu Blog leo imevinjari na kupata taswira kadhaa za mji wa Lindi.



Licha ya Mkoia huu kuanzishwa tangu mwaka 1971 ukiwa na ukubwa wa eneo Kilometa za mraba 67,000 km². Karibu robo ya eneo lake au 18,000 km² ni sehemu ya hifadhi ya wanyama ya Selous.



Mkoa wa Lindi umepakana na mikoa ya Pwani, Mtwara, Ruvuma na Morogoro. Upande wa mashariki hupakana na Bahari Hindi.



Mkoa una wilaya sita za Lindi Mjini, Lindi Vijijini, Kilwa, Nachingwea, Liwale na Ruangwa.


Lindi mjini bado inaonekana kama vile ilivyo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kutokana na namna mji huo ulivyo na kukosa hadhi kabisa ya kuonekana kuwa ni Mkoa, waweza sema kuwa ni Mkoa ambao umesahaulika kimaendeleo jambo ambalo linawafanya wananchi pia kujongea taratibu kwa maendeleo maana hadi hivi sasa zipoi nyumba za nyasi na zilizoezekwa kwa makuti katika baadhi ya mitaa mjini.



Mito mikubwa ndiyo Lukuledi, Matando na Mavuji, yote yaelekea Bahari Hindi. Mwinuko huanza mwambaoni ukipanda hadi mita 500, hakuna milima mirefu sana.



Kuna barabara chache katika hali nzuri. Ndizo 155 km za barabara ya lami na 3567 km barabara za udongo, mara nyingi katika hali mbaya. Wakati wa mvua mara kwa mara njia ya kwenda Dar es Salaam imefungwa. Kuna matumaini ya kuboreka kwa mawasiliano na mji mkuu wa Daresalaam tangu kumalizika kwa daraja la Rufiji.



Kwa sasa barabara ya kutoka Mingoyo mpaka Dar-es salaam imekamilika kwa kiwango cha lami ni kimebaki kipande cha kilometa 60 tu kuanzia Muhoro wilaya ya kilwa mpaka kukaribia daraja la Mkapa mto Rufiji ambacho kinamaliziwa kwa kiwango cha lami.



Pana kiwanja cha ndege Lindi, Nachingwea na Kilwa Masoko. Lindi na Kilwa Masoko kuna pia bandari. Huduma za simu zipata maendeleo kiasi tangu kuanzishwa kwa simu za mkononi.



Utalii haujafikia umuhimu sana kutokana na matatizo ya mawasiliano magumu ingawa Lindi ina sehemu mbalimbali zenye uwezo wa kuwavuta watalii: Kilwa Kisiwani ndicho mji wa kihistoria wa pwani la Afrika ya Mashariki pamoja na magofu ya miji mingine ya Waswahili, Selous ni hifadhi kubwa kabisa katika Afrika, ufukoni wa mchanga ni wa kuvutia sana, nafasi za zamia majini ni tele.



Gesi imepatikana baharini karibu na kisiwa cha Songosongo imeleta matumaini ya maendeleo.



 Jengo la Ghorofa mbili la shule ya Msingi Stadium ilipo jirani na Uwanja wa Michezo wa Ilulu mkoani Lindi.
 Mikoa mingi ya Mwambao wa Pwani hukosi wachuuzi wa Madafu mitaani...
 Maji hupatikana katika visima vilivyopo katika nyumba nyingi za Mkoa huo.
 Hapa ni mjini kabisa lakini miundo mbinu ya barabara bado ni duni...
 Kidogo baadhi ya maeneo kuna lami...
 Mitaa mingi ni vumbi ...
Hapa ni stendi kuu ya mabasi yanayoenda kila kona ya mji huo wa Lindi




Edited:by Abuu

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!