Searching...
Friday, December 14, 2012

WAANDISHI WA HABARI WA DRC WATEMBELEA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA.

Mhariri Mkuu wa The Guardian on Sunday, Richard Mgamba(kushoto)akiongea na waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),wakati walipotembelea ofisi za The Guardian Limited,kwa kujifunza kwa ajili ya kujifunza namna ya kuelimisha jamii kuhusu huduma ya M-pesa inavyofanya kazi hapa nchini kupitia vyombo vya habari,wapili kushoto ni Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu ambae alikuwa mwenyeji wa wageni hao.
 Meneja wa vipindi wa Clouds TV Wasiwasi Mwabulambo(kushoto)akiwaonesha namna wanavyoandaa  vipindi baadhi ya waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),wakati walipotembelea ofisi za Clouds Media Group,mahususi kwa ajili ya kujifunza namna ya kuelimisha jamii kuhusu huduma ya M-pesa inavyofanya kazi hapa nchini kupitia vyombo vya habari.  
Mmoja wa watangazaji wa Clouds TV Ben Kinyaiya akipozi katika picha na Mwandishi wa gazeti la Antenne A la DRC Mamy Tambu. 
Mhariri Mkuu wa Clouds Joyce Shebbe, akiongea na waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),kuhusu namna wanavyofaidika na huduma ya M pesa wakati walipotembelea Ofisi za Clouds Media Group kwa ajili ya kujifunza namna ya kuweza kuelimisha jamii jinsi ya kutumia huduma ya M pesa kupitia vyombo vya habari.
Mhariri Mkuu wa Clouds Joyce Shebbe, akiongea na waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),kuhusu namna wanavyofaidika na huduma ya M pesa wakati walipotembelea Ofisi za Clouds Media Group kwa ajili ya kujifunza namna ya kuweza kuelimisha jamii jinsi ya kutumia huduma ya M pesa kupitia vyombo vya habari.
 Meneja Mahusiano wa Vodacom DRC Fanny Kazadi,akifanyiwa mahojiano.
 Mwandishi Mwandamizi wa kituo cha Televisheni cha Channel ten,Bw.Dachi Mbwana akiongea na waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),wakati walipotembelea ofisi za Africa Media Group,kwa ajili ya kujifunza namna ya kuelimisha jamii kuhusu huduma ya M-pesa inavyofanya kazi hapa nchini kupitia vyombo vya habari,wapili kushoto ni Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu ambae alikuwa mwenyeji wa wageni hao.
Waandishi wa habari kutoka Jamhuri ya Kongo (DRC),wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao wakati walipotembelea kituo cha Televisheni cha Channel ten na Magic FM, kwa ajili ya kujifunza namna ya kuelimisha jamii kuhusu huduma ya M-pesa inavyofanya kazi hapa nchini kupitia vyombo vya habari.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!