Searching...
Monday, November 5, 2012

MTIKISIKO TANESCO

 Na Mwananchi Online
TETEMEKO limeendelea kulikumba Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kutokana na mamia ya wafanyakazi wa shirika hilo kupanguliwa kama hatua ya kuvunja mtandao wa wizi na hujuma ndani yake.

Habari ambazo Mwananchi lilizipata na kuthibitishwa na uongozi wa juu wa Tanesco zinasema hadi sasa wafanyakazi 190 wa Tanesco wameshakabidhiwa barua za kuhamishwa na nusu ya watumishi hao ni katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, wafanyakazi 95 wamepanguliwa kutoka katika mikoa ya Tanesco iliyopo katika Jiji la Dar es Salaam pekee na wamehamishiwa mikoani ambako wanatakiwa wawe wameripoti katika vituo vyao vipya vya kazi ifikapo Novemba 15, mwaka huu.

Kadhalika idadi kama hiyo ya watumishi kutoka mikoani wamehamishiwa Dar es Salaam, hatua ambayo inalenga kuimarisha utendaji katika jiji hilo ambalo licha ya kuwa kitovu cha uchumi wa nchi, huduma za Tanesco zimekuwa zikilalamikiwa kuwa haziridhishi.
 
 SOURCE/SOMA ZAIDI MWANANCHI ONLINE

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!