Searching...
Friday, October 5, 2012

Azam kuzalisha ujazo mpya wa juice zake mwakani


Meneja mkuu wa  Kiwanda cha kutengeneza juice cha BAKHRESA FOOD PRODUCTS LIMITED,L Naimesh Kansara akionesha timu ya  Wapigapicha waliokuwa katika safari ya Upigaji Picha za Jumuia ya Afrika Mashariki ‘EAC PHOTO SAFARI’ walitembelea viwanda hicho ujazo mpya wa boksi za Juice ambazo Kampuni hiyo itaanza kuzizalisha mapema mwakani.

Timu hiyo ya Wapigapicha ilitembelea kiwanda hicho kwakuwa tu ni Bakhresa ni Moja ya Makampuni ya kitanzania ambayo yanafanya biashara zake pia katika Nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki.

 Akizungumzia juu ya kiqwabda hicho, Meneja Kansara, alisema kuwa kiwanda hicho ni cha kwanza kwa ubora Afrika Mashariki na ni chapili kwa Afrika (ukanda wa Sahara).

Anasema kuwa wameamua kuzalisha ujazo huo ili kukidhi makundi yote katika jamii baada ya kuzalisha pakiti ndogo ambazo ni maarufu ‘kijoti’ na licha ya kuwa hupendwa zaidi na rika lote lakini watoto wamekuwa wapenzi zaidi wa ujazo huo, pamoja na ule mkubwa wa familia. Hivyo wameona ni vyema kutengeneza na nusu yake.
 Manka akionesha pakiti hizo mpya za juice za ladha mbalimbali hadi juice ya dafu ambazo zitaanza kuzalishwa Mwakani.
 Juice zikiwa katika mpangilio unaovutia
 Mfanyakazi wa Kiwanda chya Juice za AZAM akiwa kazini katika uzalishaji.

 Kiongozi wa Msafara wa Wapigapicha za EAC, ambaye ni Mtaalam wa Masuala ya Vyombo vya Habari, Sukhdev Chhatbar (kushoto) akizungumza jambo na meneja Mkuu wa Kiwanda hicho cha Juice, Naimesh Kansara.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!