
Picha AFP
Kilimo cha mboga
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa- FAO, linasema
maendeleo endelevu hayawezi kufikiwa hadi pale njaa na utapia mlo
zitakapotokomezwa. Katika ripoti iliyotolewa Jumatano mkuu wa shirika
hilo la FAO Jose Graziano da Silva, alisema lengo la maendeleo endelevu
kamwe haliwezi kufikiwa ikiwa takriban mmoja kati ya watu saba duniani
anakabiliwa na njaa au utapia mlo . Alitoa mwito wa kuongeza uzalishaji
wa chakula na wakati huo huo kulinda mazingira ili dunia iweze kukidhi
mahitaji ya chakula kwa watu wanaokisiwa kufikia bilioni tisa ifikapo
mwaka wa 2050. FAO linasema kufanikisha lengo hilo lazima uwezekazji
katika kilimo uongezwe kwa asili mia 60 katika miongo ijayo. Shirika
hilo linaongeza kuwa robo tatu ya watu maskini duniani huishi vijijini
ambapo wengi wanategemea kilimo kwa maisha yao. Ripoti ya shirika hilo
la FAO imetolewa kabla ya mkutano ujao wa Umoja wa Mataifa
unaotazamiwa kufanyika mjini Rio De Janeiro kuanzia Juni 20 hadi 22.
Mchumi wa ngazi ya juu wa shirika hilo la chakula na kilimo duniani
aliiambia sauti ya Amerika kuwa ajenda kuu ya mkutano huo itakuwa
kutokomeza njaa duniani.
0 comments:
Post a Comment