Searching...
Wednesday, July 13, 2011

WHO yaripoti mkurupuko ya Kipundupindu na Surua nchini DRC

mama na mwanae mgonjwa
Shirika la afya duniani WHO limeripoti mkurukupo wa ugonjwa wa surua na kipindupindu kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo zaidi ya watu 2,500 wameaga dunia.WHO inasema kuwa jitihada za kukabiliana na magonjwa hayo kwa njia ya chanjo na usambazaji wa bidhaa za usafi zimetatizwa na ukosefu wa fedha.
Ugonjwa wa surua unaripotiwa kusambaa kwenye mikoa saba mashariki mwa DRC huku ule wa kipundupindu ukiripotiwa kwenye mkoa wa Kisangani ambapo umesambaa hadi mjini Kinshasa ukipitia mto Congo. Tarik Jasarevic kutoka WHO anasema kuwa kwa sasa dola milioni 9 zinahitajika kugharamia kampeni za chanjo ili kuweza kukabilina na ugonjwa wa Surua.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!