Rais Salva Kiir wa Jamhuri ya Sudan Kusini anaonyesha nakala ya katiba ya muda ya taifa yake mpya
Mpango ulio na lengo la kujumuishwa kwa taifa jipya la Sudan Kusini kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa umengo’a nanga baada ya rais wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuwasilisha ombi la Sudan kusini kwa idara zilizo na jukumu la kushugulikia ombi kama hilo.
Awali Kamati inayohusika na kujumuishwa kwa wanachama wapya kwenye Umoja wa Mataifa ilikutana kuangalia ombi hilo lililowasilishwa na rais wa Sudan Kusini Salva Kiir tarehe 9 mwezi huu wakati nchi hiyo ilipopata uhuru wake .
0 comments:
Post a Comment