
Habari kutoka serikali ya Wenzhou zinasema hadi saa saba mchana wa tarehe 25, ajali ya reli imesababisha vifo vya watu 38, na wengine 200 kujeruhiwa. Hivi sasa watu waliojeruhiwa wanatibiwa katika hospitali zaidi ya kumi mjini humo. Wataalamu 13 kutoka Beijing, Shanghai na Nanjing wamefika Wenzhou tarehe 24 kushiriki kwenye kazi ya kuwatibu majeruhi.
Baada ya ajali hiyo, rais Hu Jintao wa China na waziri mkuu Wen Jiabao walitoa maagizo mara moja, wakizitaka idara husika zifanye uokoaji kwanza, kuchunguza chanzo cha ajali, na kushughulikia vizuri kazi za baadaye.
0 comments:
Post a Comment