Searching...
Tuesday, July 26, 2011

Umoja wa Mataifa kupeleka misaada Mogadishu

             
Mtoto amekaa anasubiri chakula
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP litaanza kupeleka chakula kwa ndege nchini Somalia siku ya Jumanne,mkuu wa WFP Josette Sheeran amesema wakati wa mazungumzo ya kujadili suala la ukame Afrika Mashariki.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa chakula kufikishwa huko tangu Umoja wa Mataifa kutangaza kuwa kuna ukame katika maeneo mawili ya Somalia wiki iliopita.
Katika mkutano wa dharura mjini Roma,Italia waziri mambo ya nje wa Somalia Mohamed Ibrahim ameonya kuwa watu zaidi ya milioni 3.5 "huenda wakafariki dunia kutokana na njaa" katika nchi yake.
Makundi ya kiislamu, ambayo yanadhibiti sehemu kubwa ya Somalia, yamepiga marufuku shirika la WFP katika maeneo wanayoyasimamia.
Kundi la Al-Shabab, lenye uhusiano na kundi la al-Qaeda, limeshtumu mashirika waliyoyapiga marufuku kwa kujihusisha na siasa zaidi.
Bi Sheeran amesema msaada utapelekwa kwa ndege hadi katika mji mkuu, Mogadishu, serikali ya muda - inayosaidiwa na vikosi vya kuweka amani vya Muungano wa Afrika - inadhibiti sehemu tu ya mji mkuu.
Maelfu ya raia wa Somalia wamekuwa wakikimbia kutoka maeneo ya al-Shabab na kuelekea Mogadishu na nchi jirani za Kenya na Ethiopia kutafuta chakula.
mtoto aliyedhoofishwa na njaa
Bi Sheeran alihudhuria mkutano wa Roma - baada ya kutembelea Mogadishu na kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya.
"Tulichoona sisi watoto wanawasili wakiwa wamedhoofika kabisa wakiwa katika hali mbaya ya utapia mlo na wana nafasi ndogo - chini ya asilimia 40% - ya kuishi," alisema.

"Muhimu ni kuokoa maisha ya watu sasa. Si suala la kisiasa, hakuna nia nyingine isipokuwa kuja pamoja na kuokoa maisha."

Bwana Ibrahim alisema kuwa msaada wa chakula unahitajika zaidi katika maeneo yanayodhibitiwa na al-Shabab.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!