Rais Mwai Kibaki wa Kenya ameutaka Umoja wa Afrika (AU) ujitahidi kuhakikisha kwamba amani inapatikana katika nchi za Sudan na Somalia.
Akizungumza kwenye mkutano wa Viongozi wa nchi na serikali wa bara Afrika unaofanyika mjini Malabo, Equatorial Guinea, Rais Kibaki amewataka viongozi wa bara hilo kulalamikia hatua ya nchi za Magharibi ya kupuuza uwezo wao wa kutatua matatizo ya Afrika. Kiongozi huyo wa Kenya amesema Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linapaswa kutambua na kuheshimu nafasi ya viongozi wa Afrika katika kutatua matatizo ya bara lao.
Akizungumza kwenye mkutano wa Viongozi wa nchi na serikali wa bara Afrika unaofanyika mjini Malabo, Equatorial Guinea, Rais Kibaki amewataka viongozi wa bara hilo kulalamikia hatua ya nchi za Magharibi ya kupuuza uwezo wao wa kutatua matatizo ya Afrika. Kiongozi huyo wa Kenya amesema Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linapaswa kutambua na kuheshimu nafasi ya viongozi wa Afrika katika kutatua matatizo ya bara lao.
0 comments:
Post a Comment