Manchester United imemchukua mlinzi wa Blackburn Rovers, Phil Jones, katika mkataba wa miaka mitano unaoaminika kuwa wa thamani ya pauni milioni 17.
Licha ya Arsenal na Liverpool kutaka kumsajili kijana huyo mwenye umri wa miaka 19, hatimaye ameamua kuchezea uwanja wa Man U wa Old Trafford.
"Hii ni nafasi nadra kujitokeza maishani nami natafuta changamoto mpya", alieleza Jones kupitia wavuti ya kijamii ya Twitter.
"Ningelipenda tu kuongeza kwamba nilifurahi sana kuichezea Blackburn na siku zote nitakuwa shabiki mkubwa," alielezea.
Taarifa ya United ilielezea klabu "kilifurahishwa" na hatua hiyo ya kumsajili mchezaji huyo.
0 comments:
Post a Comment