Searching...
Wednesday, April 6, 2011

Waasi wa Libya kusafirisha mafuta

Waasi Brega
Usafirishaji wa kwanza wa mafuta kutoka eneo linalodhibitiwa na waasi mashariki mwa Libya kwa takriban wiki tatu sasa unatarajiwa kuanza.
Makundi ya upinzani nchini humo yanapanga kujaza tangi la mafuta linaloaminiwa kuwekwa karibu na mji wa Tobruk.
Hatua hiyo inafanyika baada ya mashambulio ya anga kuripotiwa kufanywa na majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato dhidi ya wanaomwuunga mkono Kanali Gaddafi na waasi waliozunguka karibu na mji wa Brega.
Serikali ya Libya imebaki ngangari, huku kukiwa na ujumbe unaoitembelea Ulaya ukisistiza kwamba Kanali Muammar Gaddafi hatoachia madaraka.
Wakati huo huo Saif al-Islam Gaddafi, mtoto wa kiume wa Kanali Gaddafi ameiambia BBC waziri wa mambo ya nje Moussa Koussa hakuisaliti Libya kwa kwenda Uingereza.
Aliiambia BBC kuwa Bw Koussa alisafiri kwenda Uingereza kwa sababu za kiafya na alikuwa akishinikizwa kutoa madai yasiyo sahihi kuhusu serikali ya Libya katika jitihada ya kupata kinga dhidi ya kushtakiwa.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!