Takwimu za hivi punde zinaonyesha kuwa Idadi ya watu nchini India imeongezeka na kufikia bilioni 1.2, ikiwa ni sawa na kujumuisha pamoja idadi za Indonesia, Brazil, Pakistani, Bangladesh na Marekani.
Takwimu hizo zinaonyesha kuwa kati ya watu hao milioni 623.7 ni wanaume huku 586.5 wakiwa wanawake. Jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh ndilo lililoshuhudia idadi kubwa ya ongezeko la watu. Hata hivyo mji mkuu wa New Delhi ndio unasemekana kuwa na idadi kubwa ya watu nchini humo. Wataalamu wanasema idadi hiyo imeongezeka katika kiwango cha asilimia 17.64 ambacho ni cha chini ikilinganishwa na hapo awali.
Takwimu hizo zinaonyesha kuwa kati ya watu hao milioni 623.7 ni wanaume huku 586.5 wakiwa wanawake. Jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh ndilo lililoshuhudia idadi kubwa ya ongezeko la watu. Hata hivyo mji mkuu wa New Delhi ndio unasemekana kuwa na idadi kubwa ya watu nchini humo. Wataalamu wanasema idadi hiyo imeongezeka katika kiwango cha asilimia 17.64 ambacho ni cha chini ikilinganishwa na hapo awali.
0 comments:
Post a Comment