Searching...
Friday, April 22, 2011

Gharama za dawa za malaria zimepungua Afrika:UM

Mpango wa kimataifa wa kuhakikisha dawa za kuzuia malaria zinapatikana kwa gharama nafuu katika jamii nyingi za vijiji Afrika unapiga hatua haraka.
Wagonjwa wa malaria Afrika
Wagonjwa wa malaria Afrika
Katika nchi za Ghana, Kenya, Madagascar na Nigeria sasa dawa za kutibu malaria zinaweza kununuliwa katika maduka ya dawa na maduka binafsi kwa gharama ndogo ya dola senti 50, ikilinganishwa na mara 20 zaidi kabla ya kuanza kwa mpango huu.
Mpango huu ulianzishwa mwaka jana kwa nchi nane, ambazo ni Ghana, Kenya, Madagascar, Niger, Nigeria, Tanzania, Uganda na Cambodia ili kutoa funzo kabla kuanza dunia nzima, na matokeo yameanza kuonekana hasa katika nchi nne zilizoanza kutekeleza mapema mpango huo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!