Ushirikiano baina ya Umoja wa Mataifa na jumuiya ya nchi za Kiarabu ni muhimu sana kama kweli demokrasia itachukua mkono katika ukanda wa nchi za Kiarabu.
Katika mkutano wao ambao umejadili kwa kina hali nzima inayoendelea Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati hasa Libya, Bahrain na Yemen Ban amesema Umoja wa Mataifa utaendelea kuchukua hatua za haraka kumaliza mapigano na kutoa msaada wa kibinadamu unaohitajika.
Ameongeza kuwa ni muhimu kutumia njia za amani kuhakikisha umoja wa kitaifa, utulivu na kuweka mazingira bora ya kuleta mabadiliko.
Ameongeza kuwa ni muhimu kutumia njia za amani kuhakikisha umoja wa kitaifa, utulivu na kuweka mazingira bora ya kuleta mabadiliko.
0 comments:
Post a Comment